|
|
AS
Shk Benn amefanikiwa kupata picha ya baadhi ya vifaa ambavyo vimekwama huko Finland kwa sababu ya fedha za usafirishaji.Vifaa hivi ni idadi ya contena 3, ambazo vimetolewa kama ni msaada na vinaweza kusafirishwa mara moja kupelekwa Zanzibar pindipo kutapatikana fedha za usafirishaji contena hizo 3.
Tunaomba viongozi wa SMZ, wabunge, wawakilishi wetu, mawaziri na hata Rais wetu Dk.Karume ikiwezekana wafanikishe suala hili la usafirishaji wa vifaa hivi ambavyo vitasaidia kwenye hospitali zetu za Zanzibar.
Sisi wananchi tuko kwenye harakati za kupiga harambee, lakini gharama za usafirishaji ni kubwa na hatuna
[...]Endelea hapa “Macontena-Wananchi hima hima michango yenu inahitajika!”
Na Ali Nabwa
Marekebisho ya 11 ya katiba ya Jamhuri ya Muungano ni batili
MUUNGANO wa Tanganyika na Zanzibar ulifanywa kwa moyo thabiti wa mashirikiano mara tu baada ya kuundwa kwa umoja wa Nchi Huru za Kiafrika (OAU) Msingi wake ulikuwa na nia njema iliyojengeka tangu wakati wa vuguvugu la uhuru kwa Afrika Mashariki,Kati na Kusini (PAFMECSA)ambalo lilitambua hatima ya pamoja ya watu wa eneo hili katika vita dhidi ya ukoloni.
Kwa bahati mbaya ,shauku iliyotokana na nia njema hii iliwapelekea waasisi wa Muungano huu kufanya kosa la kihistoria la kutanguliza gari kabla ya farasi.Iliamuliwa kuunda Muungano kwanza na kushughulikia madaraka yake(katiba)baadaye.Kosa hili limewakalia wananchi wa nchi
[...]Endelea hapa “Marekebisho ya 11 ya katiba ya Jamhuri ya Muungano ni batili”
AS,
Leo kumekuwa na maoni mengi ambayo yametolewa kimakosa.Unapoingia kwenye Dashboard inakuwa sio maoni, bali ni chapisho zima jipya.
Kutoa maoni ni kubonyeza chapisho, na kuscroll down to the end utaona fomu ya kutolea maoni.
Natanguliza shukurani
Uongozi wa MZALENDO.NET
Assalamu alaykum,
Ndugu zangu kuna kiwanja kinauzwa,kiko mbweni JKT Dar es salaam.
Kina ukubwa wa square mitres 1408,kipo kwenye kilima ni view
nzuri na beach,
Kwa mwenye kuwa na intrest tafadhali wasiliana na namba hizi..
Kwa tanzania ni….0717277791.
kwa uk ni……07529591332
Kwa canada ni……01 64788662602.
Utakapo wasiliana nao hao ndio utapata maelezo zaid inshaallah
shukran…
iko siku
Hali hii ilitia wasi wasi mkubwa baada ya watu kupokea simu za kifo cha Maali Seif kuwa amesha fariki dunia, Baada ya ushunguzi wa kujuwa nani mwenye kutuma na nani wenye kutumiwa.watu walifanya upelelezi wao wa chini kwa chini na kuzi chase no, waligunduwa ni watu wenye no zao kwa njia hii au nyingine na ilikuwa ni usalama wa taifa na wengi ni wenye asili ya Bara. Kuna badhi yao walikuwa wanatuma kimakosa weye wao kwa wenye wao kufurahia kifo cha Maalim Seif pindipo atafariki. Baadhi ya sms zilikuwa zinasema pindipo akifariki huyu
[...]Endelea hapa “Break news hali ya mtafaru ilikuwa imetanda ktk visiwa vya Zanzibar huku watu wakijiweka vikundi vikundi baada ya kuskia kiongozi wao wa cuf Maalim Seif Shariff kupata ugonjwa wa hafla na kufariki Dunia.”
Na Salma Said,
HUDUMA ya nishati ya umeme iliyokosekana kwa miezi mitatu mfululizo jana imerejea katika baadhi ya maeneo Visiwani Zanzibar.
Umeme huo ambayo awali ilitangazwa kwamba utapatikana majira ya saa 9:00 kamili jioni lakini badala yake umerejea majira ya saa 11:15 huku maeneo mengi yakiwa hayajarejeshewa umeme huo ambayo umeathiri kwa kiasi kikubwa hali ya uchumi katika visiwa vya Zanzibar.
Awali akitoa taarifa kwa vyombo vya habari Kaimu Meneja wa Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) Ali Hassan Mbarouk alisema kutokana na kukamilika kwa kazi kubwa iliyofanywa na wataalamu kutoka nje ya nchi huduma ya umeme itarejea katika maeneo mbali mbali ya Zanzibar.
Meneja huyo pia aliwatahadharisha wananchi kuchukua
[...]Endelea hapa “Umeme Warejea Zanzibar”
Paka ukimfungia chumbani ukawa unampiga marungu, hakika hana budi kukujia mwilini- ndio njia pekee ya kujitetea iliobaki.
Binadamu yeyote, mateso unayompa huwa yana kikomo chake kukustahamilia. Unapomfikisha ukingoni basi huamua sasa liwe na liwalo, kusuka ama kunyoa!
Basi hii ndio hali waliyofikishwa Wapalestina, Waafghani na hata sisi Wazanzibari.
Kwa muda mrefu sana Wazanzibari walikuwa wakijua hasa kwamba mambo hayaendi kama M/Mungu mtoa uhai na mauti alivyotuumba kupata katika dunia. Wakajiuliza ni nini hasa kilichotusibu? Je ni sisi wenyewe? Ni Serikali yetu? ni kipi..!
Alhamdulillah Mola hamfichi mnafiki, mnamo karne hii mnafiki mwenyewe akamtuma mjumbe wao atangaze kuwaelezea Wazanzibari wote kwamba “Zanzibar sio nchi!”
Wakainuka waliokuwa wakidhani siku zote kwamba hawa
[...]Endelea hapa “Yalaiti Pinda asingetoa kauli….”
Na .B.OLE
Uzalendo ni kitu kinachoenda sambamba na imani, ukweli na mapenzi juu ya kitu ambacho unakipenda au kukiamini. Mara nyingi uzalendo huchukua nafasi yake kwa viumbe, ingawaje kufikia mpaka daraja ya kuitwa au kuonekana kuwa wewe ni miongoni mwa wazalendo kinadharia umefikia upeo mkubwa katika dunia hii.
Fikira, mawazo, vitendo, akili, mapenzi, imani na hata mishipa ya damu hujaa shauku ya kuamua au kutenda chochote kile ilimradi nafsi iridhike kwa kile kinachoamini katika nafsi yake.
Hapa mambo mawili yanaweza kwenda kwa uwiano, ama ukweli kwa upande mmoja au upotofu kwa upande mwengine.
Nasihi kwa vile hii sio fani yangu basi nisiende mbali,nieleze kile ambacho mara nyingi
[...]Endelea hapa “Wanzanzibar Hatuna Uzalendo ?”
Changelog:
Added fotos of Bi.Awena
Bi. Awena Sinani Masoud alizaliwa mwaka 1958 huko Wete, Kisiwani Pemba.
Mwaka 1965 – 1968 alipata elimu ya msingi katika shule ya Konde, na 1969 – 1971 alipata elimu ya sekondari katika shule ya Kizimbani huko Wete.
Mwaka 1975 aliendelea na masomo ya Kidato cha IV katika Shule ya Sekondari ya Fidel Castro huko Pemba ambapo kati ya 1976 – 1977 alijiunga na Chuo cha Ualimu cha Nkrumah.
Baada ya hapo aliaajiriwa na Wizara ya Elimu Zanzibar kama mwalimu na amewahi kushiriki katika mafunzo ya kilimo katika Kituo cha Maruhubi.
Aliwahi kufundisha katika skuli za Fidel Castro, Bububu, Migombani, Saateni, Forodhani, Jang’ombe na
[...]Endelea hapa “Mjue mke wa Maalim Seif Sharif Hamad”
Maandamano ya upinzani kuendelea Togo:
Vyama vya upinzani nchini Togo, vimesema maandamano ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa urais nchini humo, yataendelea hii leo kama ilivyopangwa, licha ya serikali kuharamisha maandamano hayo.
Msemaji wa serikali amesema, maandamano hayo yameharamishwa kwa sababu leo ni siku ya kazi. Siku ya jumamosi wiki iliyopita Rais Faure Gnassingbe, alitangazwa mshindi wa uchaguzi wa urais, matokeo
[...]Endelea hapa “Mifano ya wapinzani kupinga matokeo ya uchaguzi barani Afrika”
CCM
Sadick Mtulya
MAKAMU mwenyekiti wa CCM Bara, Pius Msekwa juzi alikaa hadi usiku wa manane katika mkutano wake na Watanzania waishio Uingereza akigawa kadi za chama hicho tawala.
Habari kutoka Uingereza zimelieleza gazeti hili kuwa katika mkutano huo Msekwa alikabidhi katiba ya CCM kwa tawi la CCM la jijini London, kadi kwa zaidi ya wanachama 70 na vifaa vingine kadhaa.
Habari zilizolifikia gazeti hili kutoka Uingereza zimeeleza kuwa Msekwa alikabidhi vifaa hivyo katika mkutano uliofanyika kwenye ukumbi wa Warehouse mjini Reanding ulioanza saa 11:00 jioni ambao pia ulihudhuriwa na balozi
[...]Endelea hapa “CCM Wajibu mapigo ya CUF-London kwa kugawa kadi za CCM Uingereza”
Azushiwa kifo, adaiwa kulishwa sumu
na Irene Mark
JANA hofu ilitanda miongoni mwa wananchi baada ya watu wasiojulikana kusambaza uzushi kwamba Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Shariff Hamad amefariki dunia, lakini Tanzania Daima lilipomtembelea hospitalini alipuuza uzushi huo na kusema, “Niko fiti.”
CUF nacho kilitoa taarifa kwa umma kikisema: “Tunawahakikishia wanaCUF na Watanzania wote kwamba hali yake ya kiafya inaendelea vizuri na daktari wake ameridhika kwamba ataweza kuendelea na shughuli za kawaida katika siku chache zijazo.”
Maalim Seif alilazwa katika Hospitali ya Hindu Mandal jijini Dar es Salaam, baada ya afya yake
[...]Endelea hapa “Niko safi ? Maalim Seif”
Salum Bimani
Hali ya afya ya Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar -Seif Sharif Hamad
Kuna hali ya wasiwasi ambayo imejitokeza kufuatia taarifa za kuugua katibu mkuu wa chama kikuu cha upinzani, CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, ambaye hivi sasa amelazwa katika hospitali moja jini Dar es Salaam.
Ili kupata kujua ukweli kuhusu hali ya Maalim Seif, Josephat Chato amezungumza na Salim Bimani, katibu mwenezi wa chama cha CUF Zanzibar ambaye kwanza alikuwa na haya ya kusema.
Mtayarishaji: Josephat Charo
Mhariri: Othman Miraji
Kumetokea ajali ya dereva wa escudo kugonga watembea kwa miguu, kutoka mwanakwerekwe mpaka kiembe samaki. wahanga si chini ya wawili wamepoteza maisha. Inasemekana kuwa dereva alikuwa na akili mbilimbili tayari.
Allah wapokee waja wako na uwasamehe dhambi zao na uwape subra wafiwa
Inna lillahi wainna ilayhi raji’uun
Na Mpitanjia wa barazani
|
|
Habari maarufu