Salum Bimani
Hali ya afya ya Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar -Seif Sharif Hamad
Kuna hali ya wasiwasi ambayo imejitokeza kufuatia taarifa za kuugua katibu mkuu wa chama kikuu cha upinzani, CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, ambaye hivi sasa amelazwa katika hospitali moja jini Dar es Salaam.
Ili kupata kujua ukweli kuhusu hali ya Maalim Seif, Josephat Chato amezungumza na Salim Bimani, katibu mwenezi wa chama cha CUF Zanzibar ambaye kwanza alikuwa na haya ya kusema.
Mtayarishaji: Josephat Charo
Mhariri:
[...]Endelea hapa “Sauti:Sikiliza mahojiano baina ya Josephat Charo na Salim Bimani”
Kumetokea ajali ya dereva wa escudo kugonga watembea kwa miguu, kutoka mwanakwerekwe mpaka kiembe samaki. wahanga si chini ya wawili wamepoteza maisha. Inasemekana kuwa dereva alikuwa na akili mbilimbili tayari.
Allah wapokee waja wako na uwasamehe dhambi zao na uwape subra wafiwa
Inna lillahi wainna ilayhi raji’uun
Na Mpitanjia
[...]Endelea hapa “Ajali mbaya Zanzibar”
Ndugu zangu WAZANZIBARI,
Mwenzenu simshirika wa mambo yanayoambatana na siasa za kwetu zanzibar lakini kama mzanzibari naguswa na mambo ya kisiasa au ya kawaida kwa zanzibar.
SIASA ndugu zangu zinatupeleka siko Zanzibar na siasa za aina hii zimetuathiri na zitaendelea kutuathiri.Athari ya siasa za aina hii hatuwezi kamwe kuziona kwa sasa kwa urahisi,lakini vizazi vyetu tunawaandalia nini?
KWANINI IWE NI U-CCM AU U-CUF tu zanzibar uekwe mbele ya kila jambo. Tukumbuke safari ya maisha yetu ni ndefu na fupi sana.
SABABU YA KUSEMA HAYO,MWENZENU NAJIULIZA SANA MASWALI YAFUATAYO: NAOMBA MNISADIE JAWABU.
1.Kwa nini Zanzibari watu wanavutana SANA kisiasa na hivyo kuwafanya wahasimiane,wapigane na watesane kisiasa?
2.kwanini iwe ni Zanzibar tu yenye
[...]Endelea hapa “TUNAELEKEA WAPI? TUMEKOSA NINI? NA DAWA YAKE NINI?”
Irene Mark
FATMA binti Baraka, maarufu kwa jina la Bi Kidude, ni miongoni mwa wasanii wanawake wachache ambao ni magwiji wa muziki wa taarabu nchini, ambaye kwa siku ya leo ataibeba manowari yetu ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo huadhimishwa kila mwaka ifikapo Machi 8.
Bibi huyu mwenye sauti nzito na inayopenya vyema masikioni mara anapoimba, ni mzaliwa wa Zanzibar lakini asili ya kabila lake ni Mmanyema kutoka Mkoa wa Kigoma, magharibi mwa nchi.
Licha ya kuwa na umri mkubwa (113) , sauti ya Bi Kidude bado ni nzuri na yenye kuvuta hisia, hasa kwa mpenzi wa miondoko
[...]Endelea hapa “Bi Kidude: Hazina ya wanawake wa Tanzania”
Habari maarufu