Login



Fotos

Get the Flash Player to see the slideshow.

Bomani? rekebisha matamshi yako wewe. hayo ni madini ya Tanganyika na yatawanufaisha wenyewe WaTanganyika sisi wazanzibar ikiwa ni sehemu ya Muundano wa Tanzania hatunufaiki chochote na madini yenu kwanza hayamo ktk Muungano? nisawa na yetu mafuta Mh Mansour kufuta rasmi ktk Muungano ,

Jaji Bomani: Madini yatainufaisha Tanzania

na Irene Mark

MWENYEKITI wa Tasnia ya Uziduaji, Jaji Mark Bomani, amesema Tanzania itaanza kunufaika na madini yaliyopo baada ya kuanza kazi kwa tasnia hiyo ya kimataifa.

Jaji Bomani, alisema sekta ya madini itaanza kuwanufaisha Watanzania wengi baada ya kuanza kazi rasmi kwa tasnia hiyo yenye kazi ya kuhakiki mapato yatokanayo na madini kwa manufaa ya wananchi.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana muda mfupi baada ya kutiliana saini waraka wa makubaliano kati ya mwenyekiti wa tasnia ya uziduaji na Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, kwa niaba ya serikali, Jaji Bomani aliwataka wananchi kutarajia neema.

Kusainiwa kwa makubaliano hayo kutasaidia kamati

[...]Endelea hapa “Bomani? rekebisha matamshi yako wewe. hayo ni madini ya Tanganyika na yatawanufaisha wenyewe WaTanganyika sisi wazanzibar ikiwa ni sehemu ya Muundano wa Tanzania hatunufaiki chochote na madini yenu kwanza hayamo ktk Muungano? nisawa na yetu mafuta Mh Mansour kufuta rasmi ktk Muungano ,”

Je tumejitayarisho kwa mvua za El Nino?

Je tumejitayarisho kwa mvua za El Nino?

Na Ally Saleh

Dunia imepiga hatua kubwa za maendeleo katika miaka ya karibuni. Kila
kitu sio tu kiekuwa rahisi lakini pia kiko katika ncha za vidole vyetu
kwa kutumia kukua kwa elimu ya kompyuta na pia utaalamu wa elimu za
jiografia na fizikia kukuwa kupita kiasi.

Kwa sasa kwa elimu hiyo mambo mambo sio tu yanaweza kubashiriwa, si
kwa njia ya ramli, lakini kwa njia ya kutumia hesabu na vigezo mbali
mbali na kwa hivyo elimu ya mwanadamu imeongezeka sana na mwanadamu
anaweza kumudu mazingira yake kwa ubora zaidi.

Miaka michache nyuma, dunia iliambiwa kuwa kutokana na kuchafuka kwa
mfumo wa kidunia basi

[...]Endelea hapa “Je tumejitayarisho kwa mvua za El Nino?”

HALI YA MAALIM SEIF INAENDELEA VIZURI

Date::3/11/2010
Watu 3,000 wapiga simu kujua kama Maalim Seif amekufa

Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad akisoma gazeti la mwananchi jana katika hospitali ya Shree Hindu Mandal ya jijini Dar es Salaam. Maalim Seif aliyelazwa katika hospitali hiyo toka Ijumaa baada ya kusumbuli na ugonjwa wa mkamba (bronchitis) anatarajia kutoka leo baada ya afya yake kuimarika.

Salim Said

ZAIDI ya watu 3,800 wamepiga simu kutoka kona mbalimbali duniani kwa viongozi mbalimbali wa Chama cha Wananchi (CUF), wakitaka kufahamu kama kuna ukweli wowote kwamba Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharrif Hamad, alikuwa amefariki duni au la.

Maalim Seif alilazwa Hospitali ya Hindu Mandal iliyo

[...]Endelea hapa “HALI YA MAALIM SEIF INAENDELEA VIZURI”

MUUNGANO WETU: Tanganyika ilikufaje Zanzibar ikabaki 2

Joseph Mihangwa

KATIKA sehemu ya kwanza ya makala haya wiki iliyopita, tuliona chimbuko la migogoro na kero za Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambazo hazijapata ufumbuzi makini hadi leo.

Nilisema kuwa kuahirishwa kwa muda usiojulikana kwa uteuzi wa Tume ya Kupendekeza Katiba, ili hatimaye kuweza kuitishwa kwa Bunge la Katiba ndani ya mwaka mmoja, ili kupitisha Katiba ya Jamhuri mpya ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, kuliupokonya Muungano huo nafasi ya kujiongoza kwa dira iliyokusudiwa, na hivyo kuendeshwa kwa Amri za Rais (decrees) na hisia za ki-imla kwa matashi ya wanasiasa.

Tuliona jinsi kwa miaka 13, tangu Aprili 26, 1964 hadi mwaka 1977, Muungano huo ulivyoendeshwa na kuongozwa kwa

[...]Endelea hapa “MUUNGANO WETU: Tanganyika ilikufaje Zanzibar ikabaki 2″