|
|
Na Ben Wazir
Nataka kubariz katika maudhui yanayohusu utamaduni, mila na desturi zetu, mambo ambayo yanaonekana sio kwamba yanakwenda mrama, lakini yanaelekea kuzama.
Nimeona nizungumzie mengi ambayo yanaleta tafash na ambayo kama yataendelea bila ya kuingiliwa kati na wahusika, pamoja na jamii kwa jumla basi yatazusha balaa kubwa.
Nimeamua niliandikie suala hili kwa vikataa viwili, kimoja wiki hii ambacho kitataalak zaidi juu ya kumomonyoka kwa maadili na kitakachofuata kitagusia mengi ambayo nionavyo mie kama khatua mnasaba hazitachukuliwa basi jamii yetu kama Wazanzibari tujue fika kuwa ipo khatarini.
Inatulazim tujuwe kuwa tutakuwa arijojo tena, ile arijojo ya burtangi, ambayo baada ya kukatika uzi, ikawa inapaa na kuelekea pasipojulikana
[...]Endelea hapa “Tumewacha yetu … tumevamia ya watu”
Na Mohammed Ghassany Waziri Burhan Saadat Haji
Si vibaya ikiwa tutadokoa kidogo katika fani ya wenyewe. Katika Falsafa kuna kitu wanakiita Fallacy, ambacho Kiswahili chake kinaweza kuwa Upotofu wa Hoja. Hoja kuambiwa imepotoka haina maana kuwa hoja hiyo haitumiki. Wako mabingwa wa kuzitumia aina hizi za hoja kwa makusudi kabisa, na machoni pa watu zikapata sura ya kuonekana kuwa hoja. Kuna hoja nyengine huitwa potofu, maana huwa zimekosa dira na hivyo huenda kinyume na zinavyotakiwa hoja ziende.
Aina moja ya Fallacy ni ile inayoitwa Argumentum ad Baculum, ambayo ni aina ya hoja ijengwayo juu ya msingi
[...]Endelea hapa “Nnahum Lamukyadhibuun! Kazi yao kukanusha tu!”
Na Muhammed Said Abdallah
Bwana Msa alikuwa kasimama dirishani, anachungulia. Nje, gari ndogo imesimama mlangoni kwa jirani yake, na dereva wake kakaa juu ya daraja ya kupandia, watoto wameizunguka, wanafanya ghasia.
Bwana Msa akatulia kimya anatazama tu. Sasa, ukimwona Bwana Msa kakaa kimya, ujuwe akili yake inakwenda kama sinema, na yale mambo hafifu ambayo watu wengine huona upuuzi, kwake yeye humsawirikia mambo mengine mapya. Kwa methali, daima alikuwa akiona katika akili yake, kuwa upo urafiki mkubwa baina ya binaadamu na magari, siku zile. Maana aliona kama urafiki unakuja kwa mazoea basi watu wamezoea basi watu wamezoeana sana na magari. Ilimtulikia Bwana Msa kwamba miaka mingi imepita tangu magari
[...]Endelea hapa “Bwana Msa na urafiki wa magari”
Na Ali N. Sultan
WAZANZIBARI wameshazoea kusoma gazeti la Dira kila Ijumaa kuanzia saa 4.00 asubuhi, takriban kwa mwaka mmoja sasa.
Tuangalie kinyume cha mambo, ile hadith ya Bwana Msa. Fikiria itakuwaje maisha ya wasomaji/Wazanzibari pale itapofika Ijumaa bila ya kusoma Dira? Bila ya kuwepo Dira mitaani, kama amri ya Serikali inayofikiria kulifungia gazeti la Dira ama kwa kutumia sheria ya usajili wa magazeti na majarida au amri ya mahkama, itatimizwa?.
Kwa mujibu wa tahrir ya Dira, na habari zilizopatikana baadaye, SMZ iko mbioni kulifungia gazeti hili. Lakini nani atafaidika na uamuzi kama huo?
Sababu ya msingi hakuna, lakini ni kwa kuwa tu wakubwa hawapendezwi na mada zinazochapishwa na gazeti
[...]Endelea hapa “Zanzibar bila Dira”
Na Ali Nabwa
HIVI sasa ulimwengu unaadhimisha mwaka mmoja wa maafa ya Tsunami, maafa ambayo Chama Cha Mapinduzi,CCM,kiliyafurahia sana kiasi ya kuyafanya kigezo cha ushindi wake katika uchaguzi uliomalizika punde hivi,kwanza Zanzibar na baadae Tanzania nzima.
Chama Cha Mapinduzi kina sifa moja,kikise! ma kitafanya maovu amini kitafanya kweli.Tsunami tumeiona na tunaendelea kuiona.Watu wa Piki,Kaskazini Pemba,na Tumbatu Chwaka,Kaskazini Unguja,bado wamo katika gharika ya Tsunami ya Mkapa na Karume.Hakuna anayejali,kwani huu ni sehemu ya mkakati maalum wa Judeo-Christian axis (mtandao wa Mayahudi na Wakristo,hivyo haishangazi kua Mayahudi ndio makungwi wa vitimbi vya Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar) ‘kuumaliza’ Uislam.Zanzibar ni kitovu cha Uislam katika Bara la Afrika na mkakati ulianza
[...]Endelea hapa “Mipango ya wayahudi dhidi ya uislamu Zanzibar”
Na J. Hussein
HISTORIA ya Zanzibar kwa kiasi kikubwa imehusishwa na biashara ya utumwa. Bahati mbaya ni kwamba wengi wa waandishi wa historia hiyo wameunasibisha utumwa na Uislamu. Katika makala hii mwandishi wetu SAID MZEE anatuelezea juu ya historia ya utumwa katika Zanzibar.DUNIA imepata kupitiwa na mifumo mingi ya maisha katika mwanadamu kutaka kuishi maisha bora kwa lengo la kuzalisha mali . Moja kati ya njia hizo ni utumwa.
Utumwa ulikuwako katika nchi zote duniani kuanzia za Ulaya, Asia hadi Afrika. Kwa mujibu wa Tarekh wazungu ndio waliokuwa watu wa mwanzo kuwafanya wazungu wenzao kuwa watumwa baadaye wakafuatiwa na Wachina.
Chanzo cha utumwa katika jamii zote kilikuwa aidha kushindwa
[...]Endelea hapa “Zanzibar na biashara ya utumwa”
Na Ali Nabwa
MCHANGA wa Kisiwandui ulitanda kuanzia kwa Ali Ahmed Riyami (Ami yake Salim Ahmed) kwenye ‘corner’ kuendea Weles (SAFI Building, pembeni ya Transworld House sasa) hadi muembeni kwa Adu ambapo Ali Ahmed alijenga baadae na kuhama kutoka kwenye ile nyumba ya miasumini, na kwa Dharamsi, mlangi – langini, kwa Bi Panya.
Ukitoka kwa Dharamsi, unapanda kilima cha Kisima Majongoo kuelekea Gongoni. Hiyo ndio Kisiwandui na ilikuwa na mikasa yake na vituko vyake.
Hapo zilikuwa zikipigwa ngumi kati ya Kisiwandui (pamoja na Kikwajuni) na Malindi. Yaani mechi zikipangwa rasmi. Wakipigana mbele ya Msikiti Mabati, pembeni ya Majabalini (nyumba inayotizamana na kibla cha msikiti).
Shujaa wa Malindi alikuwa Ba Manga.
[...]Endelea hapa “Mchanga wa Kisiwandui -II”
Na Aboud Maalim
JANA tulizungumza juu ya mtu kutoogopa kuomba msamaha kwa Mwenyezi Mungu kwa makosa aliyoyafanya. Asihisi mtu kafanya makosa akaona aibu ya kuyabeba makosa yale kwenda kwa Mwenyezi Mungu kuomba maghfira.
Tukasema namna gani kwa ushahidi wa aya mbali mbali na hadithi za Mtume namna Mwenyezi Mungu alivyo mwepesi sana kuwasamehe waja wake waliomkosea, alumuradi tu kwanza wakubali wamekosa; pili, wakubali Mwenyezi Mungu peke yake ndiye mwenye uwezo wa kuwasamehe na kuwakubalia toba zao.
Lakini hakuna ugumu wa Mwenyezi Mungu kusamehe, kwa sababu Mwenyezi Mungu hafaidiki na kitu kwa kumtesa mja wake, wala hapungukiwi na chochote kwa kumpa thawabu mja wake. Mtume (SAW) anasema:
Mwenyezi Mungu yuko tayari
[...]Endelea hapa “Kumuomba radhi binaadamu mwenzako”

Rais wa Finland, Tarja Kaarina Halonen akikagua gwaride la heshima la Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Zanzibar juzi kwa ziara ya siku moja. (Picha na Mpiga Picha Wetu).
Na Ali Nabwa
SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepeleka Bungeni katika kikao kilichoanza wiki hii, mswada ambao unapingana na Tume iliyoundwa kujaribu kutatua mzozo wa miaka mingi kati ya Umoja wa Ushirika wa Tanzania (TFC) na vyama vitano vya ushirika Zanzibar.
Mswada huo unaojulikana kama The Financial Laws (Miscellaneous Amendments) Act, 2003 unahusu Marekebisho ya Sheria
[...]Endelea hapa “Serikali ya Muungano yateka nyara mzozo wa WASHIRIKA”
suala hili khasa. Au wizara hizi zimekwisha kuunganishwa, Bara na hapa?”
“Khalafu anakataa kuwa hakuhudhuria sherehe za utiaji saini wakati sote tunakumbuka kumuona katika TVZ akiwekwa amewekwa pembeni kabisa huku wakubwa wakitiliana saini,” alisema Milo
Alimuomba Rais Amani aliangalie tena suala hili ili haki itendeke kwa Zanzibar.
Mkaazi mmoja wa Chuini, Unguja, Mzee Suleiman Makame, ambaye amesema amefanya kazi katika utafiti wa awali wa maliasili ya mafuta Zanzibar, uliofanyika kijiji cha Kama katika miaka ya Khamsini, aliliambia Dira kuwa ameshangazwa sana kusikia mafuta ni suala la Muungano.
“Yote hii ni ghilba ya
kutaka tubaki maskini. Mbona dhahabu, almasi na mengine hayamo katika Muungano?” aliuliza, na kuongeza, “Lengo ni kutubana Zanzibar
[...]Endelea hapa “Wazanzibari waja juu kwa mafuta”
Page 1 of 912345»...Last »
|
|
Habari maarufu