Login



Fotos

Get the Flash Player to see the slideshow.

Burundi yaongoza kwa ulaji rushwa

Burundi imeipiku Kenya kwa kuwa nchi yenye rushwa zaidi katika Afrika Mashariki.

Kwa mujibu wa taarifa ya hivi karibuni ya shirika la Transparency International kuhusu suala la rushwa katika nchi za Afrika Mashariki, shirika hilo limetaja Mamlaka ya Kodi ya Burundi kuwa taasisi yenye kugubikwa zaidi na rushwa katika ukanda huu, ikifuatiwa na jeshi la polisi la nchi hiyo.

Jeshi la polisi la Kenya ambalo liliongoza kwa vitendo vya rushwa mwaka jana, katika ripoti ya sasa limeshika nafasi ya tatu.

Rwanda ndiyo nchi yenye matukio machache ya rushwa ikilinganishwa na nchi nyingine za Afrika Mashariki.

Shirika hilo liliwahoji watu elfu kumi mia tano katika nchi za Rwanda,Burundi, Kenya, Tanzania na

[...]Endelea hapa “Burundi yaongoza kwa ulaji rushwa”

Chuki kwa wageni yafukuta Afrika Kusini

Jeshi lasaidia kuondoa Xenphobia

Jeshi la Afrika Kusini limeungana na polisi, kulinda doria mjini Johannesburg kutokana na mashambulio ya chuki dhidi ya raia wa kigeni yaliyosababisha watu saba kujeruhiwa vibaya.

Miongoni mwa waliojeruhiwa ni wahamiaji kutoka Zimbabwe na Msumbiji, pamoja na waafrika weusi wa Afrika Kusini waliojikuta katika mashambulio hayo jana usiku.

Katika barua kwa Rais Jacob Zuma, mkuu wa chama cha Democratic Alliance upande wa Western Cape, Hellen Zille alibaisha chimbuko la chuki dhidi ya wahamiaji weusi au Xenophobia. Hata hivyo hofu yake ilipuuzwa na mkuu wa polisi kama iliyokosa msingi.

Lakini sasa hivi imebainika wazi kuwa wageni kutoka Zimbabwe, Msumbiji, Malawi na Nigeria, miongoni mwa nchi nyingine, wanakabiliwa

[...]Endelea hapa “Chuki kwa wageni yafukuta Afrika Kusini”

Kampeni za uchaguzi nchini uholanzi (wale makaburu wa afrika kusini)

Mchakato mzima wa uchaguzi nchini uholanzi hivi ndio unavyokwenda.Hapo kwa wale wasiofahamu lugha nitajaribu kutoa madondoo mawili matatu ya sera za mwana siasa aliepo pichani.

Mchoro 1.
“Meer Veiligheid, Minder Immigratie” yaani Usalama zaidi, punguzo la wageni.

Mchoro 2.
#Nederlands velig yaani Uholanzi ilio salama, PVV (chama cha siasa hicho) kinasema kitasafisha safisha kila kitu na kufukuza na kuhamisha materorist (kwa maana ya waislamu) na wahalifu wote kutoka nchini uholanzi.

#Minder immigratie yaani punguzo la wageni, ongezeko la wageni litatugharimu fedha nyingi mabilioni ya Euros.

#Stop de islamisering
Zuia uislamu unatuletea vilemba na vishungi na maninja tuu…uhalifu jihad etc.

[SinglePic not found]
[SinglePic not found]

Anyways translation kutoka lugha moja kwenda nyengine

[...]Endelea hapa “Kampeni za uchaguzi nchini uholanzi (wale makaburu wa afrika kusini)”

Uamuzi wa mahakama za Kadhi wapingwa Kenya

Mwanasheria mkuu wa Kenya amesema atakata rufaa dhidi ya uamuzi wa mahakama ukisema kuwa mahakama za kiislamu, “Kadhi” si halali.

Siku ya Jumatatu, majaji watatu walisema mahakama hizo zinaupendelea Uislamu zaidi ya imani nyingine, na kwamba ilikuwa kinyume na katiba kwa kuwa Kenya ni nchi isiyotawaliwa katika misingi ya kidini.

Mahakama za kiislamu zimezua ubishani mzito katika katiba mpya iliyopendekezwa nchini humo.

Mahakama za Kadhi- zilizoanzishwa wakati wa utawala wa kikoloni wa Mwingereza – aghlabu hushughulikia masuala ya ndoa na urithi kwa Waislamu wachache waishio Kenya.

Mwanasheria huyo Amos Wako amesema uamuzi huo peke yake ni kinyume na sheria na unatoa mfano mbaya.

Serikali ya Kenya akiwemo Bw Wako inaiunga mkono

[...]Endelea hapa “Uamuzi wa mahakama za Kadhi wapingwa Kenya”

Mahakama za Kiislamu Kenya ‘batili’

Jopo la majaji limeamua kwamba, kuwepo kwa mahakama za kiislamu nchini Kenya ni kinyume cha sheria na inaleta ubaguzi.

Majaji hao watatu wamesema mahakma hizo maarufu kama “mahakama za Kadhi” zimeipendelea Uislamu zaidi ya imani nyingine, na kwamba ilikuwa kinyume na katiba kwa kuwa Kenya ni nchi isiyotawaliwa katika misingi ya kidini.

Mahakama za kiislamu zimezua ubishani mzito katika katiba mpya iliyopendekezwa nchini humo.

Katiba hiyo inatarajiwa kupigiwa kura ya maoni mwezi Agosti mwaka huu.

Mahakama za Kadhi- zilizoanzishwa wakati wa utawala wa kikoloni wa Mwingereza – aghlabu hushughulikia masuala ya ndoa na urithi kwa Waislamu wachache waishio Kenya.

Makanisa nchini Kenya yalifikisha malalamiko yao kuhusu suala hilo mahakamani miaka sita

[...]Endelea hapa “Mahakama za Kiislamu Kenya ‘batili’”

Ajali ya ndege yaua 104 Libya

Picha inayoonesha safari ya ndege hadi ajali

Maafisa nchini Libya wamesema ndege ya abiria imeanguka katika uwanja wa ndege mjini Tripoli na kuua takriban watu 104.

Ndege hiyo inayomilikiwa na shirika la ndege la Afriqiyah ilikuwa safarini kutoka mjini Johannesburg, Afrika Kusini.

Maafisa wamesema ilianguka wakati ikjaribu kutua karibu na uwanja huo.Takriban abiria 93 walikuwa ndani ya ndege hiyo aina ya Air Bus 330.

Watu hao wanaaminika kutoka mataifa mbalimbali zikiwemo nchi za Uingereza na Afrika Kusini.Wafanyikazi 11 wa ndege hiyo wameripotiwa kuwa raia wa Libya.

Ndege hiyo ilitarajiwa kuelekea eneo kwenye uwanja wa ndege wa Gatwick mjini London

[...]Endelea hapa “Ajali ya ndege yaua 104 Libya”

Mifano ya wapinzani kupinga matokeo ya uchaguzi barani Afrika

Maandamano ya upinzani kuendelea Togo:
Vyama vya upinzani nchini Togo, vimesema maandamano ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa urais nchini humo, yataendelea hii leo kama ilivyopangwa, licha ya serikali kuharamisha maandamano hayo.

Msemaji wa serikali amesema, maandamano hayo yameharamishwa kwa sababu leo ni siku ya kazi. Siku ya jumamosi wiki iliyopita Rais Faure Gnassingbe, alitangazwa mshindi wa uchaguzi wa urais, matokeo ambayo

[...]Endelea hapa “Mifano ya wapinzani kupinga matokeo ya uchaguzi barani Afrika”

Gordon Brown atubu kwa niaba ya Uingereza

Waziri Mkuu wa Uingereza Bw. Gordon Brown

Waziri mkuu wa Uingereza, Gordon Brown anatarajiwa kuomba msamaha rasmi kwa namna Uingereza ilivyo warejesha watoto zaidi ya laki moja katika koloni zao za zamani.
Hatua hiyo ya Uingereza ilichukuliwa chini ya mpango wenye utata wa kuwarejesha makwao wahamiaji miaka arobaini iliyopita.

Watoto wengi walichukuliwa kutoka kwa familia zao kwa nguvu na kupelekwa nchini Australia, Canada na nchi nyingine za Jumuiya ya madola.

Inasemekana badala ya watoto hao kupata maisha bora, waliteswa kwenye makao ya kuwatunza na walilazimishwa kufanya kazi ngumu kwenye mashamba.

Waathiriwa sitini wamerejea mjini London kushuhudia Waziri

[...]Endelea hapa “Gordon Brown atubu kwa niaba ya Uingereza”

Harusi ya wanaume yavunjwa Mombasa

Polisi katika mtaa wa Mtwapa ulioko kaskazini mwa mji wa Mombasa nchini Kenya wamewakamata wanaume wawili waliokuwa wanajiandaa kuoana.

Afisa wa utawala katika eneo hilo George Matundura amesema wanaume hao walikuwa na pete tayari kufunga ndoa katika hoteli moja iliyoko Kikambala katika wilaya jirani ya Kilifi.

Raia pia wameripotiwa kuwakamata wanaume wengine kadha wanaodaiwa kushiriki mapenzi ya jinsia moja na kuwakabidhi kwa Polisi.

Ndoa za watu wa jinsia bora ni marufuku nchini Kenya, lakini sio jambo la kawaida wale wanaofanya hivyo kukamatwa.

Makundi ya Waislamu na Wakristo katika eneo hilo walifanya maandamano wakilaani kile walichokielezea kuwa tabia ya baadhi ya watu isiyokubalika katika eneo hilo la

[...]Endelea hapa “Harusi ya wanaume yavunjwa Mombasa”

Afrika Kusini yaadhimisha miaka 20 tangu Nelson Mandela aachiwe huru

Nelson Mandela na mke wake Winnie baada ya kuachiwa huru hapo Februari,1990.

Nelson Mandela na mke wake Winnie baada ya kuachiwa huru hapo Februari,1990.

Großansicht des Bildes mit der Bildunterschrift: Nelson Mandela na mke wake Winnie baada ya kuachiwa huru hapo Februari,1990.

Hii leo inaadhimishwa miaka 20 tangu rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, mzee Nelson Mandela, aachiwe huru kutoka jela ya kisiwa cha Robin ambako alizuiliwa kwa miaka 27.

Kuachiwa kwake ndio uliokuwa ufunguo wa utawala wa walio wengi nchini humo.

Ili kupata picha halisi ilivyo Afrika

[...]Endelea hapa “Afrika Kusini yaadhimisha miaka 20 tangu Nelson Mandela aachiwe huru”

Page 1 of 612345...Last »