Login



Fotos

Get the Flash Player to see the slideshow.

majimbo ya bububu na mji kongwe yesema NDIO

Majimbo ya Mji mkongwe na Bububu yasema ndio..

Matokeo zaidi kufuatilia usiku mzima

[...]Endelea hapa “majimbo ya bububu na mji kongwe yesema NDIO”

Mseto wachemka Zanzibar

na Hassan Shaaban, Zanzibar

WANANCHI wa Zanzibar kesho wanatarajiwa kuandika historia mpya pale watakaposhiriki kupiga kura ya maoni kuunga mkono au kukataa serikali ya umoja wa kitaifa.

Hii ni mara ya kwanza kwa wananchi wa visiwa vya Unguja na Pemba kupiga kura ya aina hiyo tangu Zanzibar kupata uhuru wake kwa njia ya mapinduzi mwaka 1964.

Tume ya Uchaguzi Zanzibar imesema maandalizi ya kura hiyo yamekamilika na usambazaji wa vifaa katika vituo vyote vipatavyo 1,300 Unguja na Pemba utaanza leo.

Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano cha tume hiyo, Idrisa Haji Jecha, amesema vifaa kwa ajili ya kura hiyo tayari vimewasili Zanzibar kutoka Afrika Kusini na vitasambazwa leo katika

[...]Endelea hapa “Mseto wachemka Zanzibar”

Wapemba washauriwa kusahau yaliyopita

Wakati Wazanzibari wakijiandaa kupiga kura ya maoni kuamua kama Serikali ya Umoja wa Kitaifa iundwe ama la Jumamosi wiki hii, Mwenyekiti wa Kamati ya Watu sita ya Baraza la Wawakilishi inayofuatilia suala hilo, Ali Mzee Ali, amewataka wananchi wa Pemba kukataa kufitinishishwa kwa sababu za tofauti za kiitikadi.

Akizungumza katika mkutano wa pamoja wa madiwani na masheha wa Mkoa wa Kusini Pemba, Ali ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wawakilishi, aliwaambia kwamba siasa za fitina, chuki na uhasama zinahitajika kuzikwa na kujenga mustakabali mpya Zanzibar wenye kuzingatia umoja na mshikamano.

“Msikubali kufitinishwa mkapoteza watu wazuri kama ilivyotokea huko nyuma…nakuombeni sana msikubali kurudi katika balaa, tunahitaji umoja na

[...]Endelea hapa “Wapemba washauriwa kusahau yaliyopita”

Maalim Seif Akabidhiwa Zan ID Mpya

Na Salma Said,

MGOMBEA wa rais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama Cha Wananchi (CUF) Maalim Seif Sharif Hamad amesema ana matumaini ya kura ya maoni itakayoamua kuundwa kwa seirkali ya umoja wa kitaifa itafanikiwa kwa zaidi ya asilimia 52 kutokana na wananchi walio wengi wa zanzibar kuonekana kuunga mkono suala hilo.

Maalim Seif aliyasema hayo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukabidhiwa kitambulisho kipya cha Mzanzibari Mkaazi (Zan ID) chenye usajili namba namba ID 030114469 na mke wake Awena Sinani Masoud chenye usajili namba ID 199976376 na Mwanasheria wa Idara ya Ofisi ya Vitambuliho vya mzanzibari makazi Hamid Haji Machano Mtoni Mjini Unguja.

Watu wengine

[...]Endelea hapa “Maalim Seif Akabidhiwa Zan ID Mpya”

Kamati: Wapemba epukeni fitina za kiitikadi

WAKATI wananchi wa Zanzibar wakijiandaa kwa kura ya maoni itakayofanyika Jumamosi, Mwenyekiti wa Kamati ya watu sita ya Baraza la Wawakilishi inayofuatilia suala hilo, Ali Mzee Ali amewataka wananchi wa Pemba kukataa kufitinishwa kwa sababu za tofauti za kiitikadi kisiasa.

Akizungumza katika mkutano wa pamoja wa madiwani na masheha wa Mkoa wa Kusini Pemba jana, Ali ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wawakilishi alisema siasa za fitina, chuki na uhasama zinapaswa kuzikwa na kujenga mustakabali mpya Zanzibar wenye kuzingatia umoja na mshikamano.

“Msikubali kufitinishwa mkapoteza watu wazuri kama ilivyotokea huko nyuma…nakuombeni sana msikubali kurudi katika balaa, tunahitaji umoja na amani zaidi kwa hivyo ni matarajio yangu kuwa

[...]Endelea hapa “Kamati: Wapemba epukeni fitina za kiitikadi”

ZEC yaonywa kuchezea matokeo Zanzibar

ZEC

na Hassan Shaaban, Zanzibar

VIONGOZI wa vyama vya siasa na wasomi Zanzibar wameionya Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) isije ikachezea matokeo ya kura ya maoni itakayopigwa Jumamosi.

Onyo hilo walilitoa jana wakati wa wakijadili mada juu ya dhana na mtazamo ya kijamii juu ya serikali ya umoja wa kitaifa, ambapo walisema ZEC ni sawa na mwamuzi wa soka ambaye hapaswi kuruhusu magoli ya kufungwa kwa mikono.

Walisema kama tume hiyo itachezea matokeo ya kura za maoni, kuna kila dalili kwa visiwa hivyo kuingia kwenye matatizo makubwa kuliko yale yaliyomalizika hivi karibuni.

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha siasa

[...]Endelea hapa “ZEC yaonywa kuchezea matokeo Zanzibar”

Mawaziri wakabiliwa na ushindani Zanzibar

Mawaziri katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) wamekabwa koo kutokana na kuibuka kwa sura mpya za wanasiasa wanaotaka kuwania ujumbe wa Baraza la Wawakilishi katika majimbo yao.

Hali hiyo imedhihirika wakati zoezi la utoaji fomu za kuomba kuteuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwania nafasi hiyo, likimalizika leo.

Uchunguzi wa Nipashe umebaini kuwa baadhi ya majimbo yanayoshikiliwa na Mawaziri kumejitokeza idadi kubwa ya wanachama, wengine wakionekana kukubalika zaidi.

Waziri wa Nchi Afisi ya Waziri Kiongozi, Hamza Omar Juma amepata wapinzani wanne katika jimbo la Kwamtipura, tangu kuanza kutolewa fomu za kuwania nafasi hiyo juzi.

Hata hivyo, Juma anajigamba kuwa, “hata wachanganye kura zao zote waliojitokeza kunipinga, hawana ubavu wa kuniangusha

[...]Endelea hapa “Mawaziri wakabiliwa na ushindani Zanzibar”

‘Kuna shetani wa uchaguzi Zanzibar’

DAWA ya kuondoa shetani wa uchaguzi Zanzibar ni mfumo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa, imeelezwa.

“Zanzibar shetani mkubwa ni uchaguzi … shetani huyu huwa anatusumbua sana. Huyu shetani sasa tumwondoe kabisa hapa Zanzibar, tuendeshe siasa kwa kushirikiana na mimi nitapiga kura ya ndiyo siku ya kura ya maoni kwa maslahi ya Wazanzibari wote,” amesema Spika wa Baraza la Wawakilishi, Pandu Ameir Kificho.

Kificho ameyasema hayo leo alipozungumza kwenye mkutano wa siku moja ulioandaliwa na Kamati ya Watu sita ya Baraza la Wawakilishi kuhusu kura ya maoni.

Alisimulia alivyokuwa akipata taabu wakati wa mivutano ya kisiasa hata kusababisha baadhi ya wananchi kususiana maziko na shughuli nyingine za kijamii kuwa

[...]Endelea hapa “‘Kuna shetani wa uchaguzi Zanzibar’”

ZEC ipo tayari kura ya maoni

ZEC

TUME ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), imesema iko tayari kuendesha kura ya maoni mwishoni mwa wiki ijayo, kuhusu mfumo mpya wa utawala visiwani hapa wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa.

“Tuko tayari. Kampeni ya kuelimisha wananchi imekuwa ikiendelea vyema katika vyombo vya habari, kupitia mabango barabarani na vipeperushi,” alisema Ofisa Habari Msaidizi wa Tume hiyo, Salha Mohamed Ali, jana.

Alisema mashirika kadhaa yasiyo ya kiserikali yameombwa kutoa elimu kwa umma, hasa kwa makundi ya walemavu, vijana na viongozi wa dini kupitia makongamano, semina na matamasha, kuhusu kura hiyo itakayoendeshwa Julai 31 mwaka huu.

White Star Society kutoka Kaskazini

[...]Endelea hapa “ZEC ipo tayari kura ya maoni”

Afya ya Dk. Bilal yazua hofu Zanzibar

sheni-bilal

  • Mwenyewe atoa majibu uchunguzi wa afya yake

ZIKIWA zimesalia takriban wiki sita kabla ya kuanza kwa kampeni za Uchaguzi Mkuu, afya ya mgombea mwenza wa urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Mohamed Gharib Bilal, imezua mjadala ndani na nje ya chama hicho, Tanzania Daima Jumatano imebaini.

Gumzo la chini chini juu ya afya ya Dk. Bilal liliibuka ghafla kwa mara ya kwanza kutoka kwa baadhi ya wana CCM wenyewe wakiwamo wabunge na vigogo wa chama hicho, alipojitosa kutafuta tiketi ya kuwania urais wa Zanzibar mwaka huu.

Hata baada ya kuteuliwa kuwa mgombea mwenza wa Rais

[...]Endelea hapa “Afya ya Dk. Bilal yazua hofu Zanzibar”

Page 1 of 12512345102030...Last »