|
|
- Hamuamini Mkewe Kwa Sababu Hakumkuta Bikira
- Nikaah na Shariyah Zake
SWALI:
Assalam alaikum.mimi ni kijana na nina mke na watoto.lakini tangu siku ya harusi yangu nimekuwa sina uaminifu kwa mke wangu. kwa sababu siku ya kwanza ya harusi yetu wakati tunafanya tendo la ndoa nimehisi kama mke wangu hayuko bikra. na nimejaribu kumuuliza nani alombikiri kaniapia kama hajawahi kufanya tendo la ndoa kabla ya mimi, na ananihakikishia kama hajawahi kabisa kuwa na mwanamme hasa. na anasema itakuwa mimi ndo niliyemuharibu bikra yake kwa sababu nilipimuingilia siku ya kwanza nilitumia vidole badala ya uume wangu. sasa nataka kujua kweli inawezekana bikira ikaondoka kwa kutia vidole au kwa njia yoyote isiyokuwa
[...]Endelea hapa “LEO NI IJUMAA TUJIFUNZE UISLAM WETU KATIKA NDOA ZETU”
Na Ally Saleh
Kama kuna jozi ambayo tunaweza kuita ni ovu duniani basi haitashinda kwa njia yoyote ile jozi ambayo inajumujisha mambo mawili – choyo na husda. Ni jozi ambayo ina nguvu sana na ni adui kupita kiasi kwa mwanadamu.
Mwanadamu amechimbwa, ameliwa na amezikwa na jozi hii lakini katu naye ameshindwa kuepukana nayo hata kwa maonyo ya aina zote na ndio maana tukaaona kuna haja ya kuizungumzia katika makala hii hivi leo.
Ni mwanadamu ndie anaedhurika na choyo na husda kwa sababu choyo na husda hukusudiwa kutendewa mwanadamu na mwanadamu mwenziwe kwa kuwa wao ndio wenye hisia ya kujua kuwa wametendewa na wenzao.
Itokeapo choyo au husda kuhusishwa
[...]Endelea hapa “Elewa choyo na husda ni jozi ovu”
Na Ally Saleh,
Binaadamu ni kiumbe dhaifu sana. Kwa maumbile yake tunaweza kusema hakina nguvu isipokuwa wingi wa majigambo. Hakuna ubavu isipokuwa ni wingi wa tammbo. Ni kiumbe dhaifu katika viumbe vyote vilivyopewa nguvu na Muumba kuweza kukanyaga ardhi na kutoka hatua moja kwenda kwengine.
Labda hii nguvu ya kutoka kituo hiki kwenda kwengine, na kwa hivyo pia nguvu ya kunyanyua hiki kile inakuwa inampa jeuri kuwa ana uwezo na uwezo huo kumpa moyo wa kuamini kuwa anaweza kufanya lolote lile.
Si rahisi kumuona binaadamu ambaye hakaribia kutakabur kwa sababu ya kujiona ana nguvu, ana uwezo wa kufanya alitakalo, dhidi ya
[...]Endelea hapa “Ogopa bakora ya Mungu”
Na Ally Saleh
Kila siku ya maisha binaadamu ana jambo na nafsi yake. Ndio anayofikiri nayo ndio anayopanga nayo, ndio mshauri wake wa kila jambo- zuri na baya, dhaifu na imara. Ndie mwandani wake mkubwa kuliko kitu chengine chochote.
Nafsi hawezi kuikimbia kwa sababu ni sehemu yake. Ni yeye mwenyewe ndie nafsi yake. Ni sehemu iliyokaa ndani ya kiwiliwili chake na kwa kuwa imemganda, basi hana budi nayo kama asivyobudi na vitu vingi vyengine.
Na kila nafsi ina chapa ya mtu mmoja na haifanani kabisa na nyengine kama zilivyo alama za vidole au viini tete vya wanaadamu. Kwa hivyo kila nafsi ina mtizamo, fikra na misimamo yake ambayo itakuwa
[...]Endelea hapa “Ipende nafsi, usiendekeze”
Na Ally Saleh,
Maisha ni zawadi kubwa ambayo Mwenyeenzi Mungu amempa kiumbe chake mwanadamu kikiwa ndio kiumbe kilichotukuzwa kuliko vyengine vyote ambavyo viko chini ya milki yake ambayo ina ukubwa na utajiri kuliko binaadamu anavyoona anajua.
Ingawa maisha kwa mwanadamu ni sehemu ndogo sana ya utukufu wake, lakini sio wengi katika sisi tunaolijua hilo kwa kuona kuwa tunatuta, damu yetu inakwenda basi tunaringa na kuringia hayo maisha ambayo ni tunu tu tumepewa, kwa sababu kama Muumbaji asingetaka kutuumba tusingekuja katika dunia yake, mana hayupo wa kumhukumu.
Ni sehemu ndogo kwa sababu viko viumbe vyengine kwa mamilioni, ambavyo tumevijua na tunavijua, na ambavyo vinazidi kuvumbuliwa hata hivi sasa,
[...]Endelea hapa “Usiishi kwa kuishi tu, ishi kwa dhamira”
Na Ally Saleh,
Binaadamu anaishi kwa matumaini. Hii ni kwa sababu ameumbwa awe na matumaini. Mashine yake ya maisha inaendeshwa kwa matumaini, mafuta ya mtambo wake huo ni matumaini na ufundi wa mashine hiyo ni matumaini.
Kila sekunde, dakika, saa na siku ni ya matumaini. Matumaini ndio matumaini yake maana bila ya matumaini hawezi kuwa na matumaini ya kuishi na matumaini ya kufikia matumaini yake.
Nani kati yetu anaeweza kuishi bila ya matumaini? Ukisita kutumaini kwa sekunde moja tu ina maana kuwa huna tena matumaini ya kuishi na kama huna matumaini ya kuishi unaishi vipi na utaishi kwa matumaini gani?
Matumaini ni matakwa, matumaini ni tamani, matumaini ni malengo, matumaini
[...]Endelea hapa “Tuishi kwa matumaini, maana ndio sifa ya mwanadamu”
Na Ally Saleh
Leo katika safu yetu tutazungumza kitu chenye dhana pana na ambayo bahari yake ni kubwa lakini sisi tutachagua kuogelea maji madogo kwa kukhofu kuzama katika kina kikubwa. Na somo letu litakuwa juu ya maadili, lakini hili tutalifanya katika upana wake zaidi.
Maadili yanayowaongoza binaadamu yametengenezwa na wao wenyewe na madhumuni yake ni kuwawekea hao wanaadamu adabu ambazo zitasaidia uhusiano wao ambao kama hauna taratibu mara huingia tirivyogo kwa kawaida ya wanaadamu na kuzushasuitafahamu ambazo wakati mwengine hupelekea kutokea madhara.
Utengenezaji wa maadili si kitu ambacho kimezuka tu. Kama adabu hilo inatokana na mazoea ya muda mrefu ya matendeano baina ya watu na hatimae kubagua, kupembua na
[...]Endelea hapa “MAADILI NI SPIDI GAVANA KATIKA JAMII”
Na Ally Saleh
Umuhimu wa kuishi na kuendelea kuishi na hatimae kufikia tamati au khatma ya maisha yako kama ambavyo Muumba anavyoataka ni jambo amblao
lika binaadamu analitamani. Kila mtu anapenda kila kitu kimuendee kadri ya kiasi chake.
Kila mmoja wetu anapenda mambo yake yote yawe yanamnyookea. Kila kitu chake haki kinakwenda sawa, ingawa ingekuwa kama kilivyopangwa, lakini
wakati kikitokea yeye huwa hajui kuwa hiyo ni kwa mujibu wa mpangaji.
Wengi wetu hulalamika sana na hata kujisahau na kutoa maneno yasiostahiki iwapo mambo yetu yatapata upinzani hapa na pale,
matarajio kucheleweshwa kwa njia hii au ile au kujikuta tusipopapenda ingawa huwa hatujui kuwa pengine kuna kheri yetu.
Si aghlabu kutukuta
[...]Endelea hapa “Kila kitu kiwe ni kwa kiasi”
|
|
Habari maarufu