Login



Fotos

Get the Flash Player to see the slideshow.

Migawanyo

Kumbukumbu

Nyamaza kama hujui

Kwanza nimefurahi kuwa kuna mtu mwengine amejitokeza kutaka kujua “Ni Nani Mzanzibari”. Lakini bwana Mafrosty na wenziwe sijui khasa wana siri gani kuwa hamtaki suala hili watu kulizungumzia.
Kama tunataka Haki na Sawa basi nguzo zake kubwa ni uwazi katika nyombo vya khabari ikiwemo mtandao. Sasa ikiwa wewe na wenzio kazi yenu kuondosha makala za watu kwa sababu huzipendi na kutoa sababu kama Ah! zitasababisha matatizo au kuwa mtu hajui kuandika na inakubidi wewe ufanyie uratibu ni sababu za kijinga na kipuuzi.
Kwanza khasa wewe umetoka pango gani kutaka kufanyia marekebisho makala zinazoandiwa kwenye mtandao? Kazi kubwa itakupata ndugu yangu. Nchi kubwa kubwa kama China na

[...]Endelea hapa “Nyamaza kama hujui”

Je hii Democracy au Hypocracy

Mheshimiwa unanaehusika na tovuti hii nimeshangazwa sana na uamuzi wako wakuitoa nakala yangu niyoiandika kwenye tovuti hii yenye kichwa cha habari kinachosema “wakati umefika kwa Sulatani kurudi Zanzibar.

Nilivyofahamu mimi hii ni sehemu ambayo mtu yoyote anaweza kutoa mawazo yake ili watu wengine wachangie mawazo yao, kwa njia hiyo itasomesha yule alietoa mada na wale wanaochangia.

Sasa kuiondoa nakala yangu umenishangaza sana au unataka tuzungumze kuhusu Seif, Kikwete na Karume tu kwenye web site hii.

Kumbuka huwezi kuizungumza Zanzibar bila ya Sultan wa Zanzibar, hatuwezi kuikimbia history.

Nimetuma nakala ile ili nione wazanzibar wanahisi vipi kuhusu Sultan, na wewe umewanyima wazanzibari hao haki yao ya kutoa maoni yao

God

[...]Endelea hapa “Je hii Democracy au Hypocracy”

Habari zinazoboa

Assalam alaikum wachangiaji wa bodi hii

Mimi sio mwanachama wa muda mwingi katika hii tovuti(web site).Lakini kwavile ni mtanzania na mzanzibari nimeona bora na mimi nichangie mawazo yangu

Kitu kinacho niudhi mimi nikuona kuwa habari zote zinazochangiwa kwenye hii web site ni za magazetini kama si Ippmedia, basi itakuwa mzalendo nk.

Huu mtindo wa kuchukua tag na kuibandika kwenye hii web site ili wanachama wa web site hii wasome ndio unaboa, kila mtu anaweza kusoma habari za magazeti ya internet, kila mtu anaweza ku copy and paste kutoka kwenye wesite moja kwenda nyengine

Mara nyingi huwa najiuliza kweli hawa wanachama wa tovutii hii hawana mawazo yao isipokuwa yale yaliyoandikwa kwenye

[...]Endelea hapa “Habari zinazoboa”

HESHIMA – KUANDIKA NA KUCHANGIA HOJA

Nafikiri ukumbi huu umeweza kuwavutia watu wengi, kike kwa kiume Wazanzibari na Watanganyka na jirani wengine.
Naomba tuzungumzie siasa, Uchumi na maendeleo. Vikwazo katika kufikia maendeleo, maelekezo, vigenzo na uelimishaji juu ya mambo kadha yahusuyo jamii yetu.

Tuendelee ku-chati na wenzetu Watanganyika kama ni ni ndugu zetu wa damu ila malumbano juu ya kero tusitite kuambizana.

Hakuna haja ya kashfa wala matusi huo si ustaarabu wala usomi bali ni ujinga

[...]Endelea hapa “HESHIMA – KUANDIKA NA KUCHANGIA HOJA”

MTAZAMO WANGU

a/s
kwakweli huuu mtandao umeleta faraja nyingi sana katika siasa na mambo mengine kwani hata asiyejuwa siasa basi hapa atajuwa . mtazamo wangu ningeomba WAKUU WA HUU MTANDAOO watuwekeee chat room ili tuweze kupeyana mambo live live au munaiyonaje hiyo. HUU NI MTAZAMO WANGU

[...]Endelea hapa “MTAZAMO WANGU”

Maoni ya Amur

Assalam Aleykum! Tutafakari tutaifanyia nini ZNZ na Wa ZNZ . Wakati wa kuchaguwa umefika ,tutachaguwe kilicho bora ili tuondowe shida zetu.Successful Society is the product of human determination. Wakati wa kulauminiana umekwisha.Tufungue ukurasa rasmi wa Nafsi inayomtegemea ALlah! NAFSI ILIYO RIDHIKA (al-Nafs al- Mutmaina). Masomo ya akhlaq- maadili katika Islam ni mojawapo ya bora ya sayansi na inamwelekeza asomaye hadi katika elimu ya kujielewa nafsi yake mwenyewe ambayo Islam inaamini kuwa ni fardhi. Mtukufu Mtume Seydina Muhammad (s.a.w) amesema: “Yeyote yule aliyeitambua nafsi yake (mwenyewe) basi hakika ametambua Allah.”

Sisi tumuamini Mungu na tuwe na nia Swafi . Mwangaza mwema umeshaanza kuonekana. Naomba support yako na support

[...]Endelea hapa “Maoni ya Amur”

Wazalendo chagueni majina mazuri!

A/S

Ndugu zangu mimi maranyingi napenda kusoma mada na kuwangaliya maoni ya watu. lakini leo nimeona bora niwawekeeeeee wazi jinsi gani mtazamo wangu unavyoona kuwa kutumiya majina mabaya. nivyema ndugu zangu wa kislamu tupendeleeee kutumiya majina mazuri japo kuwa ni nickname lakini ningependa kutumiya jina zuri.

Kuna wachangiaji wengi hapa wanamajina wakosefu . na hata mtu anapo changiya mada basi bora achangiye kwa upeo mzuri ili asimuuzi mwezake jamani waislamu wezangu nawaomba majina haya ambayo c mazuri basi bora tubadilisheni. mimi nashidwa hata mengine kusoma maoni yao kwasababu ya jina pekeeeeee linanitiya hofu. Chaguweni nickname njema yani majina mazuri .

Ahsanteni . na samahani kama nimewaudhi na

[...]Endelea hapa “Wazalendo chagueni majina mazuri!”