Matokeo yasio rasmi NDIO inaongoza visiwani Zanzibar katika Kura ya Maoni
Ujumbe was SMS tumepokea kutoka kwa Skh Hassan wa Zanzibar
Mahojiano ya Ally Saleh na Ali Rashid
Mahojiano ya Ally Saleh na Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi Salum,Kassim
Maalim Seif apiga kura ya Maoni na kusema: “Zanzibar Daima!” (Picha kutoka FB ya Ghassany)
M.Seif akipiga kura ya NDIO (Picha kutoka FB ya Ghassany)
Wananchi wakijipanga kusubiri kupiga kura (Picha kutoka FB ya Ghassany)
Dk.Karume akitia kura ya NDIO (Picha na Ramadhan Othman Ikulu.)
Dk.Karume – kura ya NDIO (Picha na Ramadhan Othman Ikulu.)
Picha zote kutoka FB ya Ghassany Tangazo:
Kwa waliopo nyumbani tunaomba tupeane update ya kinachojiri nyumbani kufuatia Kura ya Maoni leo hii.Tafadhali acha habari hizo kama ni maoni, au kama huna internet access unaweza tuma ujumbe wa sms kwa namba 0031 684440925
Shukurani kwa ushirikiano wenu
P:S
**Tunaomba tetezi sisichapishwe kwenye machapaisho mapya kurahisisha watu kuona habari za Kura ya maoni kwenye chapisho hili ambalo litakuwa la mwanzo kwa wekeend nzima hadi mchakato huu ukimalizika.
Ikiwa zimebakia siku tatu kabla ya kufanyika kura ya maoni kuwauliza wazanzibari iwapo wanataka yawepo au la mabadiliko katika muundo wa serikali ambapo kutakuwa na serikali ya umoja wa kitaifa, kiongozi wa upinzani Maalim Seif Shariff Hamad amesema mchakato huo umewkua ukienda vizuri.
Hata hivyo Hamad alisema amefanya kazi kubwa ili kujenga mazingira ya hoja hiyo kuungwa mkono na wazanzibari wengi kwa kuwa na ridhaa nzito zaidi. akizungumza na mwandishi wetu wa zanzibar Ally Saleh alisema angetamani kura za ndio zifikie thuluthi mbili ili kumaliza tatizo la mgawanyiko wa kisiasa
Nukuu: Mahojiano ni marefu kidogo kama 38:55 minutes, hivyo faili ni kubwa linaweza kuchukua muda mrefu zaidi ya ilivyozoeleka likifanya buffering.Inategemea na Internet connection yako.
**CHA MSINGI HAPO TUJIFUNZE WASOMI WETU WA TANGANYIKA VS ZANZIBAR, NI KWELI WANATUTAKIA KHERI HAWA?
**MJADALA HUU UNAWEZA KUWA UKO NYUMA KIWAKATI, HUENDA MAADA INAYOZUNGUMZWA IKAWA HAIENDANI TENA NA HALI HALISI.SUALA LA KARUME KUONGEZWA MUDA LIMESHAPITWA NA WAKATI NA HALIPO TENA KWENYE AJENDA ZA SIASA ZA ZANZIBAR.
Kwa mara nyengine tena katika tarekh ya zama na dahari wananchi wa kijiji cha Makunduchi leo wamesherehkea mwaka mpya ambao unaelezwa kuwa una asili ya mji wa shiraz huko iran na ambao umelta usuli wa watu wanaojiita washirazi. Inakisiwa kuwa karibu nusu ya wazanzibari wanajitambulisho kuwa ni washirazi na wamektaa kuiwacha mila ya kukoga mwaka ambayo huko nchi ya asili ya iran huitwa Nairuz na hufanyika kila mwezi wa Machi na sio Julai kama huko Zanzibar. Mwandishi wetu wa Zanzibar Ally Saleh leo alikwenda huko makunduchi kusini mwa kisiwa cha Unguja na hii hapa ni taarifa yake.
Taasisi ya Mustakbali wa Zanzibar MUWAZA yenye ofisi yake London, Uingereza kwa kushirikiana na taasisi kadhaa za Zanzibar mwishoni mwa wiki iliandaa warsha ya siku mbili kujenga muelekeo juu ya suala la kura ya maoni itayopelekea Zanzibar kuwa na Serikali ya Umoja wa Kitaifa. Makala nane zilitolewa na mojawapo ilikuwa ni ya Dk Muhammed
Bakar mhadhiri wa Chuo Kiku cha Dar es salaam ambaye Ally Saleh wa BBC alizungumza nae. Kwanza alimuuliza hivi ni kweli juu ya imani kwamba
kukiwepo Serikali ya Umoja wa Kitaifa basi upinzani nao hupungua na kwa hivyo kuwa na
Mkutano mkuu wa chama tawala nchini Tanzania, CCM, uliofanyika mwishoni mwa wiki mjini Dodoma, umemalizika jana, baada ya Rais Jakaya Kikwete kutangazwa rasmi kuwa mgombea urais katika uchaguzi mkuu wa Oktoba.
Rais Jakaya Kikwete pia jana alimtangaza rasmi Dokta Gharib Billal kuwa mgombea mwenza katika uchaguzi huo wa Oktoba.
Uteuzi huo wa Dk Bilal, CCM, umekuja baada ya halmashauri kuu ya chama hicho kumchagua Dokta Ali Mohammed Shein kuwa mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM na kumuacha Dokta Bilal ambaye pia alikuwa akiwania nafasi hiyo, pamoja na wagombea wengine
Nani atakuwa mtetezi wa CCM kwa urais wa Zanzibar?
Shein, Bilal, Nahodha au Shamhuna, mtetezi wa CCM kwa urais wa Zanzibar?
Wakati huo huo, washabiki wa watetezi wanaowania kupata kibali cha uongozi wa chama tawala cha CCM kuwania nafasi ya urais wa Zanzibar katika uchaguzi mkuu wa mwezi Oktoba mwaka huu wamefika mjini Dodoma kuwapigia debe watu wanaowaona wanafaa kukamata nafasi hiyo. Watu wanaotajwa na kuzungumziwa sana kuwa huenda wakachomoza kushinda, kati ya majina 11 yaliowasilishwa kwa kamati kuu ya chama cha CCM, ni Dr. Ali Shein, makamo wa sasa wa rais wa Jamhuri ya
Mahojiano na Balozi Ali Karume juu ya mchakato wa kutafuta mtetezi wa CCM kwa urais wa Zanzibar
Mwishoni mwa wiki, kamati maalum ya Chama tawala cha mapinduzi, CCM, huko Visiwani Zanzibar ilikutana kuyajadili majina ya wanachama 11 wanaotaka kuwania nafasi ya urais wa Zanzibar katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
Kati ya majina hayo kuna waziri kiongozi wa zamani, Mohammed Gharib Bilal; makamo wa rais wa Jamhuri ya Muungano, Dr. Ali Sheni; waziri kiongozi wa sasa, Shamsi Nahodha; makamo wa waziri kiongozi wa sasa, Ali Juma Shamhuna, na Balozi Ali Karume, ndugu wa rais wa sasa wa Visiwani Zanzibar, Amani Karume.
Mtandao maarufu wa internet duniani google kwa kushikiana na chuo kikuu cha Twente huko uholanzi, kampuni ya simu za mkononi ya zantel,shirika la umoja wa mataifa la makaazi na mamlaka ya maji Zanzibar umekuwa ukiandesha mradi muhimu wa maji huko Zanzibar ambao unawezesha watumiaji kutoa taarifa ya maharibiko na kupata huduma ya haraka iwapo hawapati maji au maji ni machafu. mrtadi huo ni wa majaribio lakini tayari umeonyesha mafanikio makubwa na kuokoa muda na fedha nyingi.Afisa wa mradi huo ni Hakim Kimara. Mradi huo huitwa kwa kiingereza “human sensor web.” Ally Saleh alitaka kujua mengi kutoka kwa mratibu wa utafiti huo
Habari maarufu