Nchi yetu rudisheni, msitupige binduki

Written by  //  05/01/2010  //  Mashairi  //  2 Comments

Twataka amani, bila risasi…
Tukiwapa nafasi, mwatengeneza bunduki…
Tukiwapa ishirini, mwataka mamilioni…
Leo twasema:
Nchi yetu rudisheni, msitupige bunduki

aliye na akili, hauzi yake nchi

aliye jasiri, hatishiki kirahisi

aliye na kasi, huepuka risasi

Leo twasema:
Nchi yetu rudisheni, msitupige bunduki

asiye na mali, ni Mola hamumwamini
asiye na kazi, masaa hayampiti
asiye na jirani, ya ulimwengu ni ubishi
Leo twasema:
Nchi yetu rudisheni, msitupige bunduki

shida mitaani, twatafuta riziki

shida nchini, wenzetu wana chuki

Shida serikalini, ubaguzi hamuachi

Leo twasema:
Nchi yetu rudisheni, msitupige bunduki

Twataka amani, bila risasi…
Mamboleo ukoloni, leo hauna nafasi
Tukiwapa nafasi, mwatengeneza bunduki…
Leo twasema:
Nchi yetu rudisheni, msitupige bunduki

Wenzetu tuliwadhani, kumbe mu-nyoka mioyoni..
Ndugu zetu tulidhani, kumbe weusi wakoloni…
(Hivi kweli) Bila risasi, haiwezi kuwa amani?
Sasa twasema,
Nchi yetu rudisheni, msitupige bunduki


Chanzo:zanzinet

2 Comments on "Nchi yetu rudisheni, msitupige binduki"

  1. kombora 05/01/2010 kwa 10:27 um ·

    hengera…longa mwanangu longa.

  2. MZIMBA LIMBUKINJAGE 06/01/2010 kwa 3:37 mu ·

    TURUDISHIENI NCHI YETU YENYE MILA NA DESTURI ZAKE NAYO NI ZANZIBAR :MFUMBAVU MMOJA ALIWAHI KUTAMKA YA KWAMBA UZANZIBARI NI UDINI. KWA WALE WAZANZIBARI HII NI FAHARI YETU KWANI NDIO MILA YETU

    N:B
    Admin ameondosha makala refu-imetokeza hapa

Comments are now closed for this article.