Umoja wa Zanzibar-shairi

Written by  //  30/01/2010  //  Mashairi  //  Zima maoni

Assalaam Alaykum

kwa wanaoenda mashairi

baada ya dhiki faraja, wakuu wameamua
mambo huenda yakaja, hasama zikapungua
yaliyopita si hoja, udugu waufufua
jana tulihunzunika, leo tunafurahika

Ingawa twajikongoja, kwema twaelekea
mwanzo wa hesabu moja, kuzuri twakaribia
si lazima kwa koroja, mema sasa twasikia
jana tulihunzunika, leo tunafurahika

chuki waziweka nyuma, pamoja washikamana
furaha kubwa adhima, mioyo yatulizana
kamwe hatutosimama, kitete twashikamana
jana tulihunzunika, leo tunafurahika

mzigo wameutuwa, adui anaumia
sasa mambo yatakuwa, ya kale yatarudia
kasheshe zitapungua, jamii itatulia
jana tulihunzunika, leo tunafurahika

wakawa hawazikani, wafu wakiterekezwa
udugu na ujirani, kuyaeleza nashindwa
tafurani mitaani, vyama vikaendkezwa
jana tulihunzunika, leo tunafurahika

serikali ya pampoja, raia wahamasishwe
haki kwa kila mmoja, faraja iwasilishwe
wapemba na waunguja, jamii ziunganishwe
jana tulihunzunika, leo tunafurahika

adui ana unyoge, limemkaa kubwa donge
ilobaki ajinyonge, yakimzidi mazonge
zenji mbele isonge, sio tena kwa vivunge
jana tulihunzunika, leo tunafurahika

wa Shukran

Mohamed Al Aufi

Comments are closed.