Wananchi wakijipanga kusubiri kupiga kura

Written by  //  31/07/2010  //   //  3 Comments

Wananchi wakijipanga kusubiri kupiga kura (Picha kutoka FB ya Ghassany)

Siku imeanza Zanzibar. Ndio nimetoka kituo cha skuli ya Mtopepo ambapo Maalim Seif ndipo alipopiga kura yake kama nusu saa iliyopita. Umma ni mkubwa kwenye kituo hicho kama picha inavyoonesha. Hali kwa ujumla ni ya utulivu kwa nchi nzima. Taarifa mbaya tu ni kuwa sheha wa Mwera amewekwa ndani kwa sababu alikuwa amekaa kituoni akimwambia kila mpiga kura apige HAPANA.

3 Comments on "Wananchi wakijipanga kusubiri kupiga kura"

  1. mustaphasharif 31/07/2010 kwa 3:20 um ·

    Ndivyo tunavyoomba kila kitu kiende sawa

  2. truthtakestime 31/07/2010 kwa 4:12 um ·

    Inshallah kwa uwezo wa mungu kura ya maoni itamalizika salama na wadau watarudi nyumbani salama bila yakuwepo tokeo lolote lile linaloashiria uvunjwaji wa amani,huku mategemeo ya wengi ni kwamba kura ya NDIO ITAPITA kwa asilimia kubwa.Mungu ibariki Zanzibar,uwabariki Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla.AMIN

  3. Junius 31/07/2010 kwa 5:45 um ·

    Huyu sheha wa mwera asitolewe hadi rais mpya aapishwe.
    J

Leave a Comment

You must be logged in to post a comment.