Wananchi wakijipanga kusubiri kupiga kura
Written by Mrfroasty (Ufundi) // 31/07/2010 // // 3 Comments
Siku imeanza Zanzibar. Ndio nimetoka kituo cha skuli ya Mtopepo ambapo Maalim Seif ndipo alipopiga kura yake kama nusu saa iliyopita. Umma ni mkubwa kwenye kituo hicho kama picha inavyoonesha. Hali kwa ujumla ni ya utulivu kwa nchi nzima. Taarifa mbaya tu ni kuwa sheha wa Mwera amewekwa ndani kwa sababu alikuwa amekaa kituoni akimwambia kila mpiga kura apige HAPANA.





3 Comments on "Wananchi wakijipanga kusubiri kupiga kura"
Ndivyo tunavyoomba kila kitu kiende sawa
Inshallah kwa uwezo wa mungu kura ya maoni itamalizika salama na wadau watarudi nyumbani salama bila yakuwepo tokeo lolote lile linaloashiria uvunjwaji wa amani,huku mategemeo ya wengi ni kwamba kura ya NDIO ITAPITA kwa asilimia kubwa.Mungu ibariki Zanzibar,uwabariki Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla.AMIN
Huyu sheha wa mwera asitolewe hadi rais mpya aapishwe.
J