Usalama wa watumiaji MZALENDO.NET

Written by  //  26/02/2011  //  Ujumbe maalum  //  5 Comments

AS,

Kwanza naomba nitoe maelezo mafupi kuhusiana na IP ndio nini.IP ni anwani ya mtumiaji wa computer katika mawasiliano ya Internet.Basically, website zote ikiwemo Google,Facebook zote hizi zinaweka records za IP za watembeleaji.

Kuna upotoshaji mkubwa wa kuwa usalama wa mtu uko hatarini kwa ajili tuu unajua IP address yake.Hii dhana ni potofu na haina ukweli wowote, ndio maana siku zote nimekuwa nikikimbia kuchokora mitambo kwa ajili ya kuficha hii.Lakini naona wazanzibari tumeshajazwa khofu na woga kila kipembe, hivyo napenda kutangaza rasmi kuwa records za IP address hazihifadhiwi na mtandao wetu wa MZALENDO.NET.Hivyo hili suala la IP kujitokeza sehemu yoyote limeondoka, kama ukiliona tena tafadhali tutumie maoni tuendeleze vita dhidi ya IP.

Information ambazo mtu anaweza kujua kutoka kwenye IP ni nchi, mtoa huduma e.g Zanlink.Hapa ataishia kujua tuu kama Internet hio mtu yuko wapi lakini si zaidi ya hapo.Tusitiane khofu zisizokuwa na kichwa wala miguu.Kuhakikisha hili tembelea website hii kujua IP yako na data utakazopata au anazoweza mtu kupata http://www.easy-hide-ip.com/

Email:
MZALENDO.NET kujiandikisha si lazima kutumia email yako unaweza kutumia mfano wowote wa email e.g mrfroasty@zanzlink.com itakubalika kabisa katika mtandao wetu.Ikihitajika kuwasiliana tutapeana maoni hapa.Maana isije kuwa nafanya under estimation za watu wana khofu kiasi gani….

Passwords:
Password jisikie huru kutumia yoyote hizi ziko encrypted with md5.Hadi sasa hakuna mtu duniani alieweza kusoma md5 encryption, hivyo ukipoteza password hakuna ujanja ni lazima utengeneze password nyengine…hata ukiwasiliana na uongozi pia nao hauna uwezo wa ku-recover password, kubwa tutalofanya ni kukutengenezea password mpya ili uweze kulogin halafu ubadilishe upendavyo.

Maasalaam,
mrfroasty-technical support

Comments are closed.