Mahojiano na Balozi Ali Karume juu ya mchakato wa kutafuta mtetezi wa CCM kwa urais wa Zanzibar
Mwishoni mwa wiki, kamati maalum ya Chama tawala cha mapinduzi, CCM, huko Visiwani Zanzibar ilikutana kuyajadili majina ya wanachama 11 wanaotaka kuwania nafasi ya urais wa Zanzibar katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
Kati ya majina hayo kuna waziri kiongozi wa zamani, Mohammed Gharib Bilal; makamo wa rais wa Jamhuri ya Muungano, Dr. Ali Sheni; waziri kiongozi wa sasa, Shamsi Nahodha; makamo wa waziri kiongozi wa sasa, Ali Juma Shamhuna, na Balozi Ali Karume, ndugu wa rais wa sasa wa Visiwani Zanzibar, Amani Karume.
Othman Miraji punde hivi amezungumza na Balozi Ali Karume na kumuuliza vipi mambo yalivokwenda katika mkakati wa kutafuta mtetezi wa urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM…
Balozi Karume:
Ferus:


Sasa wewe Ali Karume ndo uwafahamishe hao CCM wenzio mambumbumbu na vyeti vyao vya kufogi wanataka mgombea mwenye shahada ya Chuo kikuu au Alietembelea chuo kikuu kwa ziara maneno yako hapo mazima Ali KARUME.
Jengine Ali karume nyinyi mnataka kufa Ikulu nini ? Hebu waachieni wenzenu na wao wapate kula yao mmekuwa ikulu toka Enzi za baba yenu sasa kaja kaka yako na wewe pia unataka hii Zanzibar yetu sote bana nasie tunataka kula vile vile. Nasema kula maana hakuna hata mmoja hapo kiongozi wa kweli na atakae kuwa muadilifu kwa wananchi wake kila atakae kuja ndo wale wale Hapa Pangu anapopaona anapataka, Hazitowafaa mali zenu wala mlichokichuma mtakwenda na Sanda ubao na Amali zenu. Mpaka yale majumba ya Michezani mmeyatowa maduka, yale majumba hayana ramani ya maduka toka enzi hizo alizozianza baba yenu . Na wewe unataka uje umalize alivyobakisha kaka yako .
Wasikilizeni viongozi wetu wanavyojikanyaga. Ali Karume mwanzo kakubali kuwa suala la kupendekezwa wagombea watano limezungumzwa ndani ya kikao. Na katoa ushahidi kuwa watu wake wanaomuunga mkono walimwambia hivyo. Baadae anaruka na kukataa kuwa hakubaliani nayo kuwa yalikuweko mambo hayo.
Bw Ferouz naye anakubali kuwa kuna CCM Zanzibar, na zaidi amewataka CCM Zanzibar ikiwa wanamapendekezo juu ya uteuzi wa mgombea urais wayapeleke. Baadae kaanza kupingana na hoja yake kwa kusema: CCM ni chama kimoja tu, hakuna CCM Bara wala CCM Zanzibar.
Naomba nimuulize Bw Ferouz ikiwa hakuna CCM Bara wala Zanzibar, vipi wewe unaitwa Naibu Katibu Mkuu upande wa Zanzibar?
Huu ndio uhodari wa viongozi wetu.
jamani jamani wazanzibar mwaka wetu huu watanganyika sasa basi mtupe tu nchi yetu hatutaki kuchaguliwa watu tusio wataka bado siku 3 tu moto uwake huko dodomaaaaaaa tushachoka tumaji nafsi zetu hatuna raha na walowezi wa tanganyika.
sheigh Ummar wewe ulimuona au kusikia fisi ameacha [mzoga] mfupa wa ZNZ wameoza akina fisi tanganyika wanao jiita TZ wanjilia au niseme wanajipgia mbwitoo wapumbavu wasio jijuwa asnte sana