|
|
Old is gold - 1
| Nimekupokea |
|
| toka__haya__nenda |
|
| WAKEREKAO |
|
| Nnamliwaza |
|
| shada__la_maua |
|
| si_lazima_-_nonini |
|
| shaba__kutu_ni_maumbile |
|
| znz_starz |
|
| Tumekinaiana |
|
| Nimezama |
|
| mtoto_kajaaliwa |
|
| usione__so_sema_nae_-taarabu |
|
| Siathiriki |
|
| niraha_ya_moyo_wangu |
|
| nabembea_nae |
|
| Wanitazama |
|
| pendo_la_moyoni |
|
| omar_koppa |
|
| Sikitiko |
|
| Track03-0 |
|
| sitaki_lawama |
|
| umasiki_wangu_-tarabu |
|
| omar_kopa |
|
| nifagilieni_____omari_kopa |
|
| viumbe_wazito |
|
| mohd_ilias |
|
| Msinilaumu |
|
| Track02-0 |
|
| unalo_lilokuka_na_roho |
|
| nimtakae_hataki |
|
| nawaseme_wasemavyo |
|
| sitaki__shauku |
|
| usiku__wa__fadhila__renew |
|
| sabalkheri__mpenzi |
|
| tumependana__kwa_siri |
|
| Mwiko |
|
| Track04 |
|
| Tunaposhikana |
|
| sabahalkheri_mpenzi |
|
| mimi__kukupenda__wewe |
|
| nina__neno__langu |
|
| umasikini_wangu |
|
| usijigambe_2 |
|
| pita |
|
| pendo__letu_la__halali |
|
| Sihiyari |
|
| mzee_yussuf |
|
| sina_bahati |
|
| Selelea |
|
|
|
Ahsante Mkuu;
Sasa hivi utawafanya Wazalendo wakumbukie zile enzi zao wakati wako Bwawani, Haelessellasi, NgomeKongwe, au Forodhanni.
Hata hivyo sinabudi kutoa maoni yangu kuhusianan na page hii.
Tunahitaji kutofautisha baina ya TAARAB na RUSHAROHO. Hivi ni vitu viwili tofauti. Kazi hii ningewaachia wenyewe kina Maalim Idd Farhan, Sh Bakar Abeid, nk, kwani wao ndio SIKIO (wengine ni ndewe tu).
Lakini ninavyo fahamu nikuwa TAARAB inatokana na neno na muziki wa kiarab hususan Misri. Ilipoiingia taarab Zanzibar, Wazanzibar waliibadilisha kidogo ili iendane na mazingira na lafdhi ya lugha ya Kishwahili.
Mwanzoni mwa miaka ya 90s, Wazanzibar haohao, waliona ipo haja ya kuboresha au kuvumbua aina mpya ya muziki wetu. Mwanzo walikuja na aina ya MODERN TAARAB. Hii haikuwa na tofauti saana na ile taarab tuliyozoweya. Kwani mashairi yalikuwa ni yaleyale yanajengeka kwa vina, mizani na vibwagizo. Pia mashairi yake yalikuwa na mfumo hulehule wa kifasihi.
Wakati ulifika, wasanii wetu mojakwamoja waliubadilisha mtiririko mzima. Walianza na kutunga mashairi amabyo ni tofauti na yale tuliyozoweya, utumiaji wa ala mpya, zaidi walibadilisha mfumo mzima wa taarab. Hapo ndio lilipozumbuliwa neno RUSHAROHO.
Ili kukuza lugha yetu ipi haja ya kuangalia kwa kina toauti hizi katika muziki wetu. Ikiwa jina RUSHAROHO haliendani, ni wakati wa wasanii wetu wa lugha kutafuta neno jengine na kulibandika katika aina hii ya muziki.
Mwisho nawaomba kadri tunavyouweleza muziki wetu hatuna budi kuonesha tofauti hii.
TAARAB ibaki kuwa ni taarab.
RUSHOROHO ibaki kuwa ni rusharoho.